Friday, August 26, 2011

East African News Agency-Disemba 2010

        
Katibu Mtendaji wa Bonde la Ziwa Victoria( LVBC), Dk. Tom Okurut aliwaambia 
washiriki wa kongamano la uwekezaji katika bonde la ziwa Victoria, mjini Mwanza:
Uwekezaji katika uendeshaji wa rasilimali ya maji utazuia uharibifu na kuimarisha 
matumizi sawa ya rasilimali hiyo, Shirika la Habari la Afrika Mashariki (EANA) 
lilimnukuu Dk. Okurut akiwaeleza washiriki wa kongamano hilo.
Wajumbe wa kongamano hilo lililojumuisha wawekezaji wa sasa
na wawekezaji watarajiwa walielezwa vivutio mbalimbali vya uwekezaji 
vilivyopo katika bonde la ziwa Victoria na jinsi gani vinaweza kuvunwa
na kubadili maisha ya watu wanaoishi kuzunguka ziwa hilo.
 Wajumbe walisema uimarishwaji wa teknolojia ya mawasiliano na habari 
utawezesha kukuza uwekezaji katika kanda hiyo.
Wakizungumzia juu ya utafiti, wajumbe hao waliitaka sekta binafsi 
na taasisi za fedha kuanzisha sera ya utafiti na maendeleo ya kanda.
Ili kukuza utalii, wajumbe walisema, kuwepo na juhudi za pamoja za kutafuta soko 
na kukuza utalii wa ndani ya Bonde la Ziwa Victoria.
Ziwa Victoria ni kubwa kuliko maziwa yote barani Afrika, 
kubwa kuliko yote katika ukanda wa tropiki duniani 
na ni ziwa la pili ulimwenguni lenye maji baridi 
likitanguliwa na ziwa Superior lilipo Amerika ya Kaskazini.
Baadhi ya vivutio vilivyomo ndani ya ziwa Victoria ni pamoja na:
kuwepo kwa visiwa 88 kati ya hivyo 48 ni visiwa vikubwa 
ambavyo vinaweza vikawa ni miongoni mwa maeneo ya utalli, 
yapo maeneo ya mapumziko na fukwe zinazoweza kuendelezwa kwa utalii 
na ipo nafasi kubwa ya kuanzishwa kwa viwanda vingi vya minofu ya samaki.















No comments:

Post a Comment